1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

UN yaonya kuhusu hatari ya kutokea magonjwa huko Gaza

30 Desemba 2023

Shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kibinaadamu OCHA, limetahadharisha hii leo kuhusu hatari inayoongezeka ya kutokea kwa magonjwa katika eneo la makaazi ya muda katika Ukanda wa Gaza.

https://p.dw.com/p/4ajJ1
Gaza: Düstere Situation für Flüchtlinge in der Region Al-Mawasi
Makazi ya muda huko Al-Mawasi kusini mwa Ukanda wa GazaPicha: DW

Eneo hilo ndiko walikokimbilia makumi kwa maelfu ya watu kutokana na mashambulizi ya mabomu ya Israel.

OCHA imesema watu hao wanaishi katika mazingira duni huku huduma za afya zikiwa zimeelemewa hasa kutokana na wimbi jipya la watu kuwasili eneo hilo kutokana na amri ya jeshi la Israel.

Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tedros Adhanom Ghebreyesus , amesena kwamba kuharisha na matatizo kwenye mfumo wa kupumua ni miongoni mwa magonjwa yanayoripotiwa katika makaazi hayo.

Takriban watu 180,000 tayari wanakabiliwa na matatizo ya kupumua huku watoto zaidi ya 136,000 walio chini ya umri wa miaka mitano wakikumbwa na magonjwa ya kuharisha. Kulingana na Wizara ya Afya huko Gaza inayodhibitiwa na Hamas, mzozo huo tayari umesababisha vifo vya Wapalestina 21,672.